Kiswahili ni lugha ya kibantu yenye misamiati mingi ya kiarabu inayozungumzwa katika eneo kubwa la Afrika ya Mashariki. Hakuna uhakika kuhusu idadi za wasemaji wa lugha; idadi zinazotajwa zinatofautiana. Wasemaji wa lugha ya kwanza wako labda kati ya milioni 7 hadi 10, na wasemaji wa lugha ya pili zaidi ya milioni sabini. Idadi ya wasemaji wa lugha ya kwanza inakua, kwa sababu lugha inaenea katika maeneo ambapo lugha nyingine zilikuwa lugha kuu, na hasa katika miji ya Tanzania imekuwepo lugha kuu, badala ya lugha za kikabila.
Kati ya nchi ambapo Kiswahili kinatumika ni Tanzania, Kenya, Uganda, Kongo-Kinshasa, Rwanda, Burundi, Msumbiji, Somalia na visiwa vya Bahari Hindi.
Swahili :: S
Tanzania :: Africa
Swahili :: Niger Kordofanian

| Kiswahili | |
| Next Video | |